Wanaienzi kazi ya kuchimba dhahabu kwa pesa za haraka wanazojipatia huku wakihatarisha maisha yao kuitafuta kwa udi na uvumba bila ya kutumia vifaa maalum na hata kutojali kemikali kwenye migodi. Wengi wamepoteza maisha yao lakini wengine wanaendelea kujivunia kingi lakini kichache. Pheona kengah alizuru migodi ya kakamega na kutuletea taarifa kuhusu azma ya kuchimba dhahabu kwenye migodi fauka ya hatari zilizoko katika makala maalum ya migodi ya kakamega.